Friday, July 13, 2012

SIKU HIZI KITAALAMU ZAIDI NA MAMBO YANAKUWA KAMA UNAVOTAKA,

UKITAKA KUZAA MTOTO WA JINSIA GANI, FANYA HIVI.
1]MWANAMKE WAPASWA KUJUA VYEMA MZUNGUKO WA SIKU ZAKO.Inafaa tufahamu kuwa ili kuweza kujua ni siku zipi za mwezi mwanamke anaweza kushika mimba (to conceive) inabidi tujua kwanza kipindi ambacho mwili wa mwanamke uko tayari kushika mimba au Ovulation Period. Ovulation ni wakati ambao yai lililokua hutoka katika mirija ya ovari katika kizazi cha mwanamke na katika wakati huu uwezo wako wa kushika mimba ni mkubwa
2]Kwa kawaida mwanamke hutoa yai lenye mbegu x ambazo ni za kike. mwnaume hutoa mbegu zenye X,Y kwa maana ya kiume na kike na Ovulation haifuati mpangilio maalum kati ya ovari katika kila mwezi na haijulikani ni ovari gani itatoa yai kila mwezi. Wakati yai linapotoka huwa na uwezo wa kurutubishwa au kukutana na mbegu ya kiume na kuanza kutengeneza mtoto kwa muda wa masaa 12 hadi 24, kabla halijapoteza uwezo wake. na Iwapo yai litafanikiwa kurutubishwa na mbegu ya kiume kwa wakati maalum na kujikita katika fuko la uzazi basi matokeo yake ni mimba. Na iwapo halitorutubisha yai hilo pamoja na kuta za kizazi huharibika na kutoka nje ya mwili kama damu ya hedhi.
3] Mzunguko wako wa mwezi ni siku ya kwanza ya hedhi hadi siku ya kabla ya kuanza hedhi nyingine. Kwa mfano iwapo nimepata siku zangu tarehe Pili Julai na nimepata tena siku zangu tarehe 29 Julai, mzunguko wangu ni wa siku 28. Kwa kawaida mzunguko wa siku 28 ndio mzunguko wa kawaida kwa wanawake wengi. Lakini kuna baadhi ya wanawake huwa na mzunguko wa chini ya siku 28 na wengine huwa na mzunguko wa hadi siku 35.
Note;Kipindi cha kubeba mimba huanza siku 4 hadi 5 kabla ya Ovulation, na humalizika masaa 24 hadi 48 baada ya hapo hii ni kwa sababu muda wa ovulation huweza kuchelewa au kuwahi kutokana na sababu mbalimbali.
4]mbegu ya kiume huwa na uhai kwa siku 4 hadi 5 na yai huweza kuishi kwa masaa 24 hadi 48 baada ya kuingia katika tumbo la uzazi. Hivyo kwa kujua siku hizo humsaidia mwanamke kufahamu kipindi chake cha Ovulation kimewadia na hivyo kuweza kukukutana na mumewe au mwenza wake wakati huo ili aweze kubeba mimba.
5]sasa Kila yai la mwanamke lina chromozu mbili za X. Iwapo manii ya mwanamume au spemu (ambayo in chromozomu X na Y) itakuwa na X na kurutubisha yai la mwanamke lenye X tupu, basi mtoto atakayezaliwa atakuwa mwanamke. Vilevile iwapo spemu ya mwanamume itakuwa na Y na kurutubisha yai la mwanamke, basi mtoto atakayezaliwa atakuwa mwanamume.
6]inakuwa hivi, mbegu za kiume n[Y] zina spidi sana nahufa mapema sana masaa machacha tu. zile za kike [X] huchelewa kufika ila zinaishi muda mrefu.
mfano wa mchanganuo wa mtoto wa kike.
• Unajamiiana siku 2 au 3 kabla ya Ovulation. Kinadharia spemu za kiume zitakuwa zimeshakufa hadi kufikia siku hasa ya Ovulation na kuziacha spemu za kike zikiwa hai tayari kurutubisha yai na kuunda mtoto wa kike.
• Anashauri pia wanawake wajizuie kufikia kileleni (orgasm) kwani hali hiyo itaufanya uke uwe na hali ya asidi ambayo ni kwa faida ya spemu ya kike yenye chromozomu X.
• Pia anawashauri wazazi wanapojamiina wawe katika hali ya mwanamke kulala chini na mwanamume juu au missionary position. Kwani anasema kuwa mtindo huo huziwezesha spemu zenye chromozamu X zimwagike karibu na mlango wa uke na kuwa na uwezekano mkubwa wa kuingia ukeni na kutungwa mimba.
MCHANGANUO RAHISI WA KUPATA MTOTO WA KIUME.
(1)-Mbegu zinazosababisha mtoto wa kiume hutoka haraka na kwa speed kubwa sana ili kuungana na Yai vilevile hufa haraka (hufa ndani ya masaa 3 ya mwanzo).

(2)-Mbegu zisababishazo mtoto wa kike hujivuuuta sana (maringo ya wanawake yanaanza b4 hata hatujawa viumbe kha! hihihihi) na hubaki hai kwa zaidi ya masaa 72 (zaidi ya siku tatu).


(3)-Bao zito na lenye afya ndio muhimu kusababisha mtoto wa kiume (mlishe mumeo lishe bora).


Hivyo basi ili kufanikisha hili unapaswa kutegea siku ambazo wewe unajua yai lako limepevuka na linasubiri kurutubishwa na mbegu ya kiume. Ukingonoka kwenye siku hatari kuliko zote ni wazi kuwa zile mbegu za jinsia ya kiume zitakuwa za kwanza kurutubisha yai na kufanya mimba ambayo itakuwa ya mtoto wa kiume.

No comments: